Kuanzia wiki iiliopita, kwenye Makao Makuu ya UM, kulikusanyika wajumbe karibu 2,000, waliowakilisha mashirika kadha wa kadha, ya wenyeji wa asili waliotokea sehemu mbalimbali za dunia, ambao walihudhuria kikao cha mwaka, cha wiki mbili, kuzingatia taratibu za kuchukuliwa kimataifa, kutekeleza mapendekezo ya ule Mwito wa UM juu ya Haki za Wenyeji wa Asili.