Harakati za kusaka suluhu kwa makumi ya mamilioni ya watu waliojikuta ni wakimbizi ndani ya nchi zao kutokana na mizozo na majanga ya kiasili zitapatiwa nguvu mpya kufuatia makubaliano mapya yaliyotiwa saini hii leo huko Geneva, Uswisi kati ya shirika la uhamiaji la Umoja wa mataifa, IOM na kituo cha kufuatilia ukimbizi wa ndani, IDMC.