Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Bangladesh unaotarajiwa kufanyika jumapili hii ya tarehe 30 mwezi huu wa Desemba, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia taarifa iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani na msemaji wake, amewasihi wadau wote Bangladesh wahakikishe wanaweka mazingira yasiyo na vurugu, vitisho wala kulazimishwa, kabla, wakati na baada ya uchaguzi, ili kuwezesha uchaguzi wa amani, halali na unaohusisha watu wote.