Miaka kumi baada ya Umoja wa Mataifa Tkutoa wito wa kuhusishwa zaidi kwa wanawake katika masuala ya amani, mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa una takwimu mchanganyiko kuhusu suala hilo na unataka juhudi ziongezwe kufikia lengo.
Umoja wa Mataifa umesema leo kuwa umefanikiwa kuinua hali ya usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake wengi kushiriki kwenye shughuli za uzalishaji kwenye sekta ya kilimo katika maeneo ya vijijini, lakini hata hivyo umesema kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili wanawake hao wafaidike na mavuno ya kazi zao .
Viongozi wa serikali kutoka Umoja wa Ulaya, kundi la wataalamu pamoja na viongozi kutoka Asia wanakutana leo huko Brussels kwa mkuatano wa siku mbili ambao utajikita kujadilia mtizamo halisi juu ya wahamiaji kutoka asia wenye shabaya ya kwenda kufanya kazi barani Ulaya.
Shirika la afya duniani WHO limesema chanjo ya mafua iliyosababisha athari za kusinzia au Narcolepsy miongoni mwa watoto na vijana haitoondolewa kwenye soko.
Nchini Sri Lanka, mvua kubwa zilizonyesha katika siku saba zilizopita zimesababisha mafuriko katika wilaya 18 zikiwemo za Mashariki, Kaskazini, Katikati, Uva na majimbo ya Kusini .
Mkuu wa tume ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Navi Pillay anatarajiwa kufanya ziara rasmi nchini Urusi na mji St. Petersburg mwezi huu kama moja ya njia ya kuboresha uhusiano na Urusi katika masuala ya haki za binadamu.