Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewataka viongozi wa dunia wanaokutana huko Davos, Uswis kwenye mkutano wa biashara kuzidisha nguvu kukabili kasi ya ukuaji wa magonjwa yasiyoambukizwa kwa nchi zinazoendelea ambayo huenda yakaongezeka maradufu hadi kufikia mwaka 2030.