Mafuriko yanayoighubika Australia hivi sasa kwa mara nyingine yanaashiria umuhimu wa nchi zote zinazoendelea na zilizoendelea kuwa na mipango imara au la kukabiliwa na athari kubwa za hali ya hewa limesema shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na kupunguza majanga UNISDR.
Umoja wa Mataifa umezindua mchezo wa video kwa kutumia wavuti kwa lengo la kuwapa vijana taarifa muhimu kuhusu kuzuia maambukizi ya HIV, huku ukiwaelimisha, kuwaburudisha na kuchagiza tabia njema zinazojali afya zao.
Msaada wa chakula kwa familia 42,000 kwenye jimbo la Bajaur nchini Pakistan umesitishwa na mpango wa chakula duniani WFP kufuatia shambulio la kujitoa muhanga siku ya Jumamosi.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amelaani shambulizi la kigaidi lililotekelezwa nje ya kituo cha kusambaza misaada cha shirika la mpango wa chakula duniani WFP mashariki kwa Pakistan ambalo lilisababisha watu 45 na kuwajeruhi wengine wengi.
Wakati kikao cha 65 cha baraza kuu la Umoja wa Mataifa kikikunja jamvi, rais wa baraza hilo Joseph Deiss amepongeza mkutano huo ambao amesema ulifungua njia ya kuongeza kasi ya kufikia malengo ya maendeleo ya milenia ya Umoja wa Mataifa na kuondokana na umasikini na maradhi yanayoisumbua dunia.
Ripoti mpya iliyotolewa leo na Umoja wa Mataifa inaonyesha kwamba usafirishaji nje wa bidhaa katika Asia na Pacific unakuwa huku viwango vya uchumi vikiongezeka kwa tarakimu mbili kwa mwaka huu wa 2010.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amekaribisha kura ya bunge la Marekani ya kuunga mkono kuidhinishwa kwa mkataba wa kupunguza zana za nyuklia uliotiwa sahihi mapema mwaka huu kati ya viongoiz wa Urusi na Marekani.
Maafisa wa Umoja wa Mataifa wameonya kwamba wapigaji wa Afghanistan Taliban wanaweza kuanzisha mkakati mpya wa kuzusha mashambulizi mapya katika kipindi cha wiki chache zijazo.