Baraza la jamii na uchumi ECOSOC limehitimisha majadiliano yake ya siku mbili ya ushirikiano wa maendeleo kwa wito wa haja ya haraka ya kuwa na mipango ya kufikia malengo ya maendeleo ya milenia hapo 2015.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu UNFPA Thoraya Ahmet Obaid amesema utamaduni ni kuhusu kuhodhi mabadiliko na hakuna mabadiliko yatakayokuja kutoka nje.