Ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Colombo nchini Sri Lanka zimefungwa baada ya maandamano. Ofisi hizo zimefungwa leo baada ya kiongozi mwenye msimamo mkali mshirika wa Rais wa Sri Lanka kuongoza maandamano makubwa nje ya ofisi hizo kwa siku ya pili akidai watakaa hapo hadi Katibu Mkuu Ban Ki-moon atakapolivunja jopo la uchunguzi wa uhalifu wa vita nchini humo.