Huku kukiwa na joto kali, ukame na moto wa nyika, sehemu nyingi za dunia zilikuwa zimepitia mojawapo ya Julai tatu zenye joto zaidi katika rekodi, limesema shirika la Umoja wa Mataifa la hali ya hewa WMO hii leo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA, limetoa ombi la dola milioni 10.7 kwa ajili ya kutoa usaidizi wa kuokoa maisha kwa wanawake na wasichana zaidi ya milioni mbili nchini Sri Lanka.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres anaendelea na ziara yake nchini Japan baada ya mapema hii leo Jumamosi kuhudhuria sherehe za kuadhimisha miaka 77 ya shambulio la mbomu la nyuklia la Hiroshima lilosababisha maafa ambayo athari zake zinaendelea kuonekana mpaka hii leo.
Ni jambo lisilokubalika kabisa kwa mataifa yenye silaha za nyuklia kukiri uwezekano wa vita vya nyuklia, Amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Maataifa Antonio Guterres, Jumamosi nchini Japan katika sherehe za kuadhimisha miaka 77 ya shambulio la bomu la nyuklia la Hiroshima.
Nchini Thailand, neema imerejea tena kwa wafugaji wa Kamba wadogo baada ya teknolojia mpya ya kuchuja maji na kulisha viumbe hao kusaidia kuondoa changamoto waliyopata awali ya milipuko ya magonjwa kutokana na uchafu wa maji kwenye mabwawa wanayofugia.
Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu na afya ya uzazi UNFPA, leo limetaja washindi 10 wa pamoja wa shindano la miradi bunifu inayoweza kuleta mabadiliko chanya na kuwezesha wanawake na wasichana duniani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO, limesema nchi zinapaswa kushirikiana kukomesha haraka kuenea kwa ugonjwa wa ndui ya nyani, au Monkeypox bila kujali utaifa, rangi ya mtu au dini, amesema afisa mwandamizi wa shirika hilo hii leo.
Wakati zaidi ya robo tatu ya watu wazima wote wanaoishi na Virusi vya UKIMWI VVU wanapata aina fulani ya matibabu, idadi ya watoto wanaofanya hivyo, inafikia asilimia 52 pekee.
Wiki ya Unyonyeshaji watoto maziwa ya mama duniani imeanza rasmi hii leo chini ya kauli mbiu yake isemayo Kuongeza Unyonyeshaji: Elimisha na Usaidizi, Umoja wa Mataifa unatoa wito kwa serikali kutenga rasilimali zaidi ili kulinda, kukuza, na kusaidia sera na programu za unyonyeshaji, haswa kwa familia zilizo hatarini zaidi ambazo zinaishi katika mazingira ya dharura.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani shambulio la leo huko nchini Afghanistan ambalo limesababisha vifo vya raia kadhaa na wengine wamejeruhiwa.