Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Ulimwenguni, WHO iliyotolewa hii leo mjini Geneva, Uswisi yenye jina 'Hali ya ulimwengu kuhusu hatua za afya ya umma dhidi ya tatizo la kusahau', inasema ni robo tu ya nchi zote ulimwenguni ambazo zina sera, mkakati au mpango wa kitaifa wa kusaidia watu walio na ugonjwa wa shida ya akili unaosababisha kupoteza kumbukumbu na hali nyingine kama kushindwa kufikiria vizuri.