Mshauri Maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu kuzuia mauaji ya kimbari, Alice Wairimu Nderitu, na Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Michelle Bachelet, leo Jumapili wametoa onyo la wazi dhidi ya hatari ya ukatili mkubwa unaoendelea nchini Myanmar, baada ya siku nyingine ya umwagaji damu ya ukandamizaji unaotekelezwa na jeshi la Burma.