Safari ya malengo ya maendeleo endelevu au SDGs alianza mwaka 2015 na kila mtu anajua wapi ni mwisho wa safari yetu, kutokomeza umasikini na njaa, usawa kwa wanawake na wasichana , kuwawezesha vijana, kupunguza hewa ukaa, kuwa na uchumi wa kukabili mabadiliko ya tabianchi, ajira zenye hadi na mafanikio ya pamoja, jamii zenye amani na haki, haki za binadamu kwa wote na kuheshimu utawala wa sheria. Pia fursa kwa wote za kuishi katika dunia bora.