Nchini Bangladesh katika eneo la kaskazini mwa nchi katika mji wa Mollikpur, mradi uliofadhiliwa na Mfuko wa Kimataifa Umoja wa Mataifa wa Maendeleo ya Kilimo, IFAD kwa kushirikiana na serikali ya nchi hiyo, umeanza kuzaa matunda kwa wanawake wa umri mdogo ambao wamepata mafunzo ya udereva.