Idadi ya waathirika wa usafirishaji haramu imeongezeka, huku idadi ya makundi yaliyojihami na magaidi wanawasafirisha wanawake na watoto kwa ajili ya kupata fedha na kuwaandikisha kama wafuasi, kwa mujibu wa ripoti ya takwimu za kimataifa kuhusu usafirishaji haramu wa watu iliyozinduliwa leo mjini Vienna, Austria.