Maafisa wakuu wa jeshi nchini Myanmar, ikiwa ni pamoja na kamanda Mkuu Min Aung Hlaing, wanapaswa kuchunguzwa na kushtakiwa kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa vita, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi na jopo huru la kiamtaifa la uchunguzi dhidi ya Myanmar.