Pamoja na kufanya kazi kubwa ya kuhabarisha umma, waandishi wa habari ulimwenguni kote wanakabiliwa na mashambulio yanayohatarisha usalama wao ambapo mashambulio hayo ni pamoja na kauli za chuki, udhalilishaji kwenye mitandao ya kijamii, vurugu, ubakaji na hata mauaji.Ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya kukomesha uhalifu dhidi ya waandishi wa habari Umoja wa Mataifa unasema muarobaini wa yote hayo ni utashi wa kisiasa.