Janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 limeongeza mara nne mahitaji ya kila siku ya hewa ya oksijeni kwa wagonjwa katika nchi za kipato cha chini na kati, amesema Philippe Duneton, Mkurugenzi wa UNITAID, ambalo ni shirika tanzu la shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO likiwa na wajibu wa kufanikisha uwepo wa tiba nafuu duniani.