Ripoti mpya ya shirika la afya ulimwenguni WHO kuhusu hali ya ugonjwa wa kifua kikuu duniani, TB inasema kuwa idadi ya watu waliougua kifua kikuu au kufariki dunia mwaka jana ilikuwa ni ndogo ingawa bado mataifa mengi hayachukui hatua za kutosha kuweza kutokomeza ugonjwa huo ifikapo mwaka wa 2030.