Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametoa wito wa kuwepo na juhudi za pamoja ili kupambana na uhalifu. Akizungumza kwenye mjadala wa baraza la usalama kuhusu vitisho vya kimataifa dhidi ya amani na usalama , amekumbusha jinsi nchi wanachama walivyoungana kukabiliana na magonjwa, umasikini, mabadiliko ya hali ya hewa na ugaidi.