Hali ya uchumi wa dunia inatazamia kukua kwa wastani mwaka ujao, lakini pia nchi za Ulaya zitakabiliwa na changamoto ya ulipaji madeni ili kudhihirisha ukuaji wa uchumi huo.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amesema kuwa mpango wa amani nchini Nepal unaendelea kukumbwa na utata huku Umoja huo ukijiandaa kuondoka nchini humo.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa na mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan balozi Rauf Engin Soysal na mratibu wa Umoja wa Mataifa nchini Pakistan Tomo Pakkala inasema mamilioni ya wapakistan bado wanahitaji msaada kukabili athari za mafuriko yaliyowakumba.
Umoja wa Mataifa leo umetangaza kuanza mpango mpya wa mashirikiano na Jamhuri ya Korea kwa ajili ya kuipiga jeki Campodia kukabiliana na tatizo la uchafuzi wa mazingira.
Mradi wa kuwapa wanawake mafunzo ambao hawana uwezo wa kupata ajira uliofadhiliwa na shirika la kuwahudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR umetajwa kuwa wenye manufaa kwa familia zao.
Shirika la mpango wa chakula duniani WFP linasema kuwa limetumia karibu dola milioni sita mwaka huu kuwasaidia watu 240,000 waliothirika na mizozo kusini mwa Kyrgzstan na wengine 340,000 katika mikoa sita kati ya mikoa saba nchini humo.
Bodi ya wakurugenzi wa shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP imeidhinisha kuongeza mwaka mmoja zaidi ya mpango wa msaada wa chakula nchini Bangladesh.
Chimbo la Ache nchini Indonesia limepiga hatua kubwa ya ujenzi mpya tangu kukumbwa na janga la tsunami miaka sita iliyopita. Hata hivyo ripoti ya Umoja wa Mataifa imeonya kwamba bado linakabiliwa na changamoto kubwa ya kuondoa umasikini, kuleta usawa na athari za majanga kwa siku zijazo.
Bodi kuu ya shirika la fedha duniani IMF juma hili imeidhinisha kuongezwa kwa muda wa miezi tisa wa kutoa mkopo kwa nchi ya Pakistan hadi mwezi Septemba mwaka 2011.