Hii Leo ikiwa ni siku ya kukabiliana na utipwatipwa au unene uliokithiri, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO, linasema ingawa siku hii ni tukio la kila mwaka, laini madhara ya janga la Corona au COVID-19 kuanzia mwaka jana yamefanya tukio hili kuwa na maana zaidi kuliko wakati wowote ule.