Haki za binadamu zimeathirika vibaya wakati wa janga la corona au COVID-19, lakini wakati huu wa kujikwamua na janga hilo ni fursa muhimu ya kuboresha hilo na kuhakikisha utu kwa wote, amesema leo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kwenye Baraza Kuu la Umoja huo.