Wajumbe na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wametandaza mikeka yao ya yoga na kujinyoosha kwa mitindo mbalimbali ya yoga, katika hafla iliyofanyika nje Jumatatu jioni kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa huko New York, kwa lengo la kusherehekea maadhimisho ya nane ya Kimataifa ya siku ya Yoga, ambayo kila mwaka huadhimishwa tarehe 21 Juni.