Watu wanaokadiriwa kuwa milioni 2.4 huenda wakaathirika na machafuko ya kisiasa nchini Ivory Coast kwa mujibu wa mashirika ya kibinadamu Afrika ya Magharibi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amerejea kusistiza msimamo wa Umoja wa Mataifa kwamba matokeo ya uchaguzi wa karibuni wa Urais nchini Ivory yanadhihirisha matakwa ya watu na hivyo matokeo lazima yaheshimiwe.
Chuo kikuu cha Nairobi nchini Kenya kwa ushirikiano na Umoja wa Mataifa kupitia ofisi yake iliyoko Nairobi UNON wamezindua rasmi programu ya kwanza kabisa ya shahada ya uzamili katika ufasiri na kutafsiri katika kanda ya Afrika ya Mashariki.