Msemaji wa KM ameripoti kwamba Ban Ki-moon leo amewatumia makundi kadha husika na tukio la Guinea, ripoti maalumu ya Tume ya Uchunguzi ya Kimataifa juu ya hatua kali za kinidhamu zilizochukuliwa na vikosi vya usalama dhidi ya raia waliokuwa wakiandamana, bila ya fujo, kwenye mji wa Conakry, mnamo mwisho wa mwezi Septemba mwaka huu, ambapo raia wanaokadiriwa 150 waliuawa, na wingi kujeruhiwa.