Wakati mwaka 2021 unakaribia, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, lina wasiwasi kuhusu afya na ustawi wa watoto milioni 10.4 wanaokadiriwa kuugua utapiamlo uliokithiri mwaka ujao katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, kaskazini mashariki mwa Nigeria, Sahel ya Kati, Sudan Kusini na Yemen. Hizi ni nchi au kanda ambazo zinakabiliwa na majanga mabaya ya kibinadamu wakati pia zikikabiliwa na ongezeko la ukosefu wa chakula, janga hatari la corona.