Katika mapambano dhidi ya Virusi Vya UKIMWI, VVU na UKIMWI nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, vikundi vya kijamii vinavyoundwa na watu wanaoishi na VVU vinasaidia kusambaza dawa katika maeneo ambayo yana ugumu wa kufikiwa kutokana na usalama mdogo na uhaba wa huduma za kiafya, juhudi ambazo zimewasaidia wengi kama ilivyo katika vijiji vya Zemio.