Ijumatano wajumbe wa Baraza la Usalama (BU), wanaowakilisha mataifa wanachama 15, walipitisha, kwa kauli moja, azimio lenye kuruhusu Vikosi vya Ulinzi Amani vya UM katika JKK (MONUC), kutumia "uwezo wote walionao", chini ya Mlango wa VII wa Mkataba wa UM, unaoruhusu kutumia nguvu, ili kuwapatia raia hifadhi wanayostahiki, dhidi ya mashambulio kutoka makundi yote yenye kuhatarisha usalama wao.