Ujumbe wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuwahudumia watoto UNICEF uliozuru maeneo ya Shadatkot na Sindh nchini Pakistan kati ya tarehe 21 na 23 mwezi huu unasema kuwa maneo ya vijiji ya sehemu hizo yameharibiwa kabisa huku wanaorejea makiwa wakikosa nyumba , chakula , shule au njia zozote za kujikimu kimaisha kufuatia mafuriko makubwa yaliyoyakumba maeneo hayo. Hadi leo UNICEF imepokea dola milioni 169 kati ya ya dola milioni 251 ilizoomba. Marixie Mercado ni msemaji wa UNICEF:
(SAUTI YA MARIXIE MERCADO)