Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA leo limesema idadi kubwa ya watu waliosambaratishwa na mafuriko nchini Pakistan ama wamerejea katika maeneo yao ya awali au wanafanya hivyo.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mawasiliano ITU na serikali ya Ureno wanashirikiana kutoa kompyuta mpakato au lap top mashuleni katika nchi zinazoendelea.
Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa viongozi wa Gunea kuhakikisha kwamba duru ya pili ya uchaguzi wa Rais inafanyika kwa amani katika taifa hilo la Afrika ya Magharibi.
Naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya mipangilio ya sera Robert Orr amesema kuwa hata kama kuna hali mbaya ya uchumi duniani jitihada mpya zinazofanywa na serikali zinaonyesha matumani ya kupunguza vifo vinavyosababishwa na Ugonjwa wa malaria ambao kwa sasa vinawaua watu milioni moja kila mwaka kote duniani na kuukomesha ugonjwa huo ifikapo mwaka 2015.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO ameelezea huzuni yake kufuatia kifo cha mwanasayansi wa Ufaransa Georges Charpak ambaye alikuwa mshindi wa tuzo ya nobel ya fizikia mwaka 1992.
Rais wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa Joseph Deiss amesema wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahitaji kuonyesha ujasiri ili kuvuka viunzi vya kufikia amani duniani.
Serikali ya Uganda imekasirishwa vikali na ripoti ya awali iliyovuja ya Umoja wa Mataifa ambayo inaishutumu nchi hiyo kwa uhalifu wa vita nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.