Vijana 3000 nchini Ivory coast, wakiwemo wapiganaji wa zamani na wanawake watapata mafunzo ya ujenzi, kazi za viwandani na sekta za huduma chini ya mradi mpya wa Umoja wa Mataifa .
Naibu mwakilishi wa Umoja wa Mataifa nchini Liberia Hnrietta Mensa-Bonsu amewapongeza maafisa wa polisi wa Rwanda wanaofanya kazi na mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo kwa utaalamu wa kazi, na nidhamu.
Naibu mwakilishi maalumu wa vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika UNAMID kwenye jimbo la Darfur Sudan Mohamed Yonis jana amezuru Kusini mwa Darfur.