Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewapongeza watu wa Jamhuri ya Tanzania na haswa visiwa vya Zanzibar kwa kupiga kura ya maoni hivi karibuni kwa amani na utulivu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewapongeza watu wa Jamhuri ya Tanzania na haswa visiwa vya Zanzibar kwa kupiga kura ya maoni hivi karibuni kwa amani na utulivu.
Wananchi wa Kenya leo wamepiga kura muhimu ya maoni kuamua hatma ya katiba mpya ya nchi hiyo, huku viongozi wakitoa wito wa kuwepo na amani kote nchini.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linaendelea kupleka misaada ya kuokoa maisha kwa mamilioni ya waathirika wa mafuriko nchini Pakistan wengi wao wakiwa watoto na wanawake.
Umoja wa Mataifa umezitaka Israel na Lebanon kujizuia kuendeleza mvutano baada ya majibizano ya risasi jana kwenye eneo linalozigawa nchi hizo mbili la msitari wa bluu.
Afisa wa zamani wa serikali ya Rwanda amehukumiwa kwenda jela miaka 25 kwa kushiriki katika mauaji ya mwaka 1994 yaliyokatili maisha ya Watutsi wengi na Wahutu wa mzimamo wa wastani nchini Rwanda.
Kamati ya umoja wa mataifa inayohusika na ukaguzi wa karibu watu 500 ambao wanastahili kuwekewa vikwazo kwa kuwa na uhusiano na makundi ya kigaidi yakiwemo ya Taliban na Al-Qaeda imeyaondoa majina 45 kutoka kwa orodha hiyo.