Mlimbwende wa kimataifa Naomi Campbell amesema alipewa mawe machafu baada ya chakula cha usiku kilichohudhuriwa pia na aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor.
Ripoti mya iitwayo malengo ya maendeleo ya milenia nchini Iraq inasema Iraq inahitaji kuongeza juhudi zaidi ili kufikia malengo hayo, yaliyoafikiwa na viongozi wa dunia mwaka 2000 ya kuimarisha hali ya maisha ya watu ifikapo 2015.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo ameungana na maelfu ya watu wa Nagasaki Japan kuweka shada la maua katika mnara wa kumbukumbu ya waliouawa mwaka 1945 kwa shambulio la bomu la atomic.
Afisa wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa haja ya kuongeza juhudi za kutatua masuala muhimu yakiwemo ya uraia na mipaka kabla ya kura ya maoni nchini Sudan.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA linasema zaidi ya watu milioni 4 wameathirika na mafuriko ya Pakistan ambayo ymeshakatili maisha ya watu zaidi ya 1600.
Wananchi wa Kenya leo wamepiga kura ya maoni ya katiba mya kwa amani na utulivu. Kura hiyo iliyoelezwa kuwa ni muhimu sana imeshuhudia idadi kubwa ya watu waliojitokeza kushiriki.
Majaji katika mahakama ya kimataifa ya the Hague wamekataza mwanamitindo maarufu Naomi Campbell kupigwa picha anapotoa ushahidi katika kesi ya aliyekuwa Rais wa Liberia Charles Taylor.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq Ad Melkert amesema Iraq imefikia mahali nyeti sana kufuatia kumaliza kwa mafanikio uchaguzi wa bunge Machi 7 na kuidhinisha matokeo ya uchaguzi huo Juni pili.