Mkurugenzi Mtendaji wa Idara ya Chakula Duniani WFP, Bi. Josette Sheeran atafanya ziara ya siku mbili huko Pakistan, kutathmini jinsi kazi za shirika lake zinavyokidhi mahitaji ya mamilioni ya watu waloathirka na mafuriko, kuhakikisha uratibu mzuri na juhudi za serikali ya Pakistan na kuhimiza kuendelea kupatikana ungaji mkono wa kimataifa katika juhudi za msaada.