UNICEF inakadiria kwamba zaidi ya watu milioni 2 wangali wanaathiriwa moja kwa moja au kwa njia nyingine na matokeo ya mtetemeko wa ardhi huko Haiti. Na watu wengine milioni 1.3 wamekoseshwa makazi yao hadi hivi sasa.
Afisi ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO imeeleza wasi wasi wake kutokana na kile kinachoaminika ni kutekwa nyara mtetea haki za binadam aliyezungumza dhidi ya ukiukaji wa haki za binadam unaofanywa na wanajeshi wa nchi hiyo.
Wakurugenzi wakuu wa Idara ya kuwahudumia watoto UNICEF na Mpango wa Chakula Duniani WFP wametoa wito kwa jumuia ya mataifa hii leo kuongeza msaada wao kwa waathiriwa wa mafuriko yanayoendelea huko Pakistan.
Idara ya Maendeleo kwajili ya Wanawake ya Umoja wa Mataifa UNIFEM, inaanda warsha mwezi mzima wa Septemba, katika wilaya saba za uchaguzi nchini Tanzania ili kuimarisha mikakati ya uchaguzi ya wagombea wanawake, kabla ya uchaguzi mkuu wa October.
Idara ya Watoto ya Umoja wa Mataifa UNICEF imeipongeza serikali ya Sudan ya Kusini kuundwa na kuzinduliwa kitengo cha kulinda watoto ndani ya Jeshi la Ukombozi wa Sudan ya Kusini SPLA, ikielezea kwamba hiyo ni hatua ya kihistoria kwajili ya haki za watoto nchini humo.
Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linakutana hii leo kuzindua rasmi Mpango wa Kimataifa wa Kuchukuliwa Hatua kupambana na biashara haramu ya binadamu. Akizungumza kwenye mkutano huo, Katibu Mkuu Ban Ki-moon anasema biashara haramu ya watu ni miongoni mwa ukiukaji mbaya kabisa wa haki za binadamu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Matifa Ban Ki-moon amewaombea heri manusuru wanaoendelea kukwama katika machimbo moja ya migodi nchini Chile akisema kuwa anaamini wataopolewa wakiwa bado salama.
Shirika la afya Ulimwenguni WHO linakadiria kwamba zaidi nusu ya milioni ya kina mama wajawazito ambao wamekumbwa na mafuriko nchini Pakistan watajifungua katika kipindi cha miezi sita kuanzia sasa.
Huko Vietnam ikizidi kupiga hatua za kimaendeleo kukabiliana na umaskini kwa miongo miwili iliyopita kumetolewa wito wa kuwepo kwa juhudi zaidi na kujumuishwa jamii maskini.