Wakati huu ambao tatizo la chakula linaongezeka katika eneo la Sahel na kuwaweka mamilioni katika hatari ya baa la njaa, shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO limeanza kugawa mbegu bora kwa wakulima nchini Burkina Faso.
Mjini Mombasa Kenya Ijumaa hii kumemalizika kongamano la kimataifa la uongozi, usimamizi na utawala bora likijumuisha washiriki kutoka sehemu mbalimbali.
Kesho Juni 26 ni siku ya kimataifa ya kuwaunga mkono waathirika wa utesaji na mataifa yote yana sheria ambazo zinapinga utesaji na kuufanya kuwa ni kosa.
Ripoti ya utafiti wa lishe ya watoto nchini Niger iliyotolewa leo inasema hali ya lishe kwa watoto nchini Niger imeshuka sana katika miezi 12 iliyopita.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeruhusiwa kuanza tena sehemu ya shughuli zake nchi Libya baada ya mazungumzo na serikali ya Libya kuhusu uamuzi wa serikali kulitimua nchini shirika hilo.
Maafisa wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wamewatembelea wakimbizi wa Kyrgystan wanaorejea nyumbani kwa idadi kubwa kutoka nchini jirani ya Uzbekstan.
Serikali ya Kenya imewaambia maharamia sasa imetosha kwa kufungua mahakama maalumu Shimo la Tewa mjini Mombasa ili kuendesha na kuhukumu kesi za washukiwa wa uharamia.