Afisa wa Umoja wa Mataifa amesema wakati haki ya utulivu imerejea katika miji ya Kyrgyzstan ya Osh na Jalal-Abad , hofu ya mivutano ya kikabila na uvumi wa machafuko unazidi.
Mcheza tennis mashuhuri ambaye ni balozi mwema wa shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP Maria Sharapova atasafiri kutoka Wimbledon ambako anashiriki mashindano hivi sasa hadi Belarus kuzuru eneo lililoathirika na zahma ya nyuklia ya Chernobyl mwaka 1986.
Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa anayeondoka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo amesema ingawa sehemu kubwa ya nchi hiyo hivi sasa ina kiasi Fulani cha amani lakini bado kuna changamoto.
Jumuiya ya wafanya biashara imetakiwa kushirikiana kujenga misingi ya kimataifa ambayo itaziweka haki za watoto katika jajenda ya juu ya ushirikiano wa jukumu la kimataifa.
Kamishna mkuu wa Umoja wa Mastaifa wa shirika la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Antonio Guterres amehitimisha ziara ya siku mbili nchi Lebanon kwa msisitizo wa kushirikiana na serikali ya nchi hiyo kuboresha maisha ya wakimbizi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea hofu yake kufuatia taarifa kwamba manispaa ya Jerusalem ina mipango ya kubomoa nyumba zilizokuwepo na kujenga makazi zaidi ya walowezi katika eneo la Silwan mashariki mwa mji huo.
Viongozi wa masuala ya biashara wametakiwa kukubaliana katika mpango wa maendeleo ambapo makampuni yatafanya kazi kwa ushirika zaidi na Umoja wa Mataifa kufanikisha mipango na miradi mbalimbali.