Mtaalamu maarufu wa masuala ya wanawake amesema tatizo la fistula na vifo vya kina mama wenye umri wa kuweza kuzaa ni kubwa kwenye jimbo la Darfur Sudan.
Ugonjwa wa sotoka unaoathiri midomo na miguu kwa wanyama umezuka katika nchi za Asia za Japan na Jamuhuri ya Korea ambazo awali zilitangaza rasmi kuwa hazina tena ugonjwa huo.
Leo ni siku ya kimataifa ya masuala ya afya na usalama kazini. Katika kuadhimisha siku hii mkuu wa shirika la kazi duniani ILO ametoa wito wa kuzuia hatari zozote zinazojitokeza katika sehemu za kazi.
Wakati huohuo utafiti wa kimataifa uliofanywa na shirika la kimataifa la nguvu za atomic IAEA unaonyesha kuwa katika baadhi ya nchi watoto wanawekwa katika hatari kubwa ya mionzi wanapofanyiwa vipimo kama CT scans.
Shirika la kimataifa la nguvu za atomic IAEA linashirikiana na Roche shirika linaloongoza katika matibabu ya saratani, kukabiliana na ongezeko la matatizo ya saratani katika nchi za Afrika zilizoko kusini mwa jangwa la Sahara.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia watopto UNICEF kwa kushirikiana na Chuo kikuu cha New School jijini New York, leo limefungua warsha kubwa kuhusu wasichana vigori.