Wanajeshi wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya congo wamewaokoa watu zaidi ya 20 waliokuwa wakisafiri kwa boti kutoka Kivu baada ya injini ya boati hiyo kuzimika.
Mwigizaji maarufu na balozi mwema wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi Angelina Jolie yuko Bosnia Herzegovina kutembelea wakimbizi wa ndani.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR chini ya mradi wake mpya limefanikiwa kuwaandikisha wakimbizi elfy 26 wa Colombia waliko kaskazini mwa Equador.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF pamoja na washirika wake wanaunga mkono wito wa wizara ya elimu ya Haiti ya kuwataka watoto warejee mashuleni.