Mawaziri wa mambo ya nchi za nje kutoka sehemu mbali mbali za dunia, akiwemo waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani Hilary Clinton, wanakutana Montreal, Canada Jumatatu asubuhi, kwa mkutano wa kimataifa juu ya namna ya kusaidia kukarabati taifa la Haiti lililoharibiwa na tetemeko la ardhi.