Imetangazwa kutoka Roma, Utaliana, leo hii, yalipo Makao Makuu ya Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) ya kuwa jamii ya kimataifa inakaribia kufyeka milele lile janga maututi la maradhi ya sotoka, ugonjwa wa kuhara wenye kuambukiza ng\'ombe, maradhi ambayo kwa muda wa miaka mingi, yalikuwa yakiwasumbua wakulima, hasa kwenye yale maeneo ya Afrika, kusini ya Sahara.