Mataifa ya Marekani, Australia, Brazil, Ufaransa, Utaliana, New Zealand, pamoja na Norway, pamoja na Usweden na Uingereza yameripotiwa kuchangisha msaada wa dawa ya chanjo kinga dhidi ya homa ya mafua ya A/H1N1, mchango ambao utasaidia pakubwa kuhudumia umma wa kimataifa.