Ashraf Qazi, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Sudan na Mkuu wa Shirika la Ulinzi Amani Sudan Kusini (UNMIS) ameripotiwa hii leo kuelekea eneo la mgogoro wa mpaka la Abyei, kwenye mkesha wa kutangazwa na Mahakama ya Upatanishi wa Abyei kutoka Hague maamuzi kuhusu eneo la mfarakano baina ya Sudan Kaskazini na Kusini. Uamuzi utatolewa na Mahakama ya Upatanishi Ijumatano. Mjumbe wa KM kwa Sudan Kusini alinakiliwa akisema hatua zimeshachukuliwa na wenye madaraka, za kuhakikisha makundi yote yenye silaha, isipokuwa Vikosi vya Pamoja vya Polisi na Jeshi, yameondoshwa kutoka Eneo la Mfarakano la Ramani ya Abyei kabla ya maamuzi kutangazwa kuzuia fujo.