Mjumbe Maalumu wa UM juu ya Masuala ya Maziwa Makuu, Olusegun Obasanjoaliyekuwa raisi wa zamani wa Nigeria, ambaye anazuru Mako Makuu kushauriana na wakuu wa UM kuhusu hali ya eneo, aliwaambia waandishi habari Ijumanne kwamba maendeleo ya kurudisha utulivu na amani katika eneo la vurugu, la mashariki katika JKK yanajikokota, hasa kwenye zile juhudi za kukomesha uhasama baina ya makundi ya waasi na vikosi vya Serikali.