Alkhamisi KM alikuwa na mkutano makhsusi na Mjumbe wa Kudumu wa Myanmar katika UM. Kwenye mkutano wao huo KM alimuarifu Mwakilishi wa Myanmar ya kuwa ni matarajio yake, na pia ya jumuiya ya kimataifa, halkadhalika, kwamba Serikali itazingatia, kwa uangalifu mkubwa zaidi, taathira za hukumu watakayotoa kwenye kesi inayomhusu kiongozi wa upinzani Aung San Suu Kyi, na anaamini Serikali itatekeleza jukumu lake adhimu la kumtoa kizuizini mapema iwezekanavyo.