Kwenye mkutano na waandishi habari uliofanyika kwenye Makao Makuu, KM Ban Ki-moon alitangaza kumteua rasmi Raisi mstaafu wa Marekani, Bill Clinton kuwa Mjumbe Maalumu wa UM kwa Haiti. Mkutano ulihudhuriwa na Raisi Clinton pamoja na Waziri wa Nchi za Kigeni wa Haiti, Alrich Nicolas. Clinton aliwaambia wanahabri ya kwamba licha ya dhoruba kadha wa kadha zilizopiga Haiti mwaka uliopita na kusababisha uharibifu mkubwa ndani ya nchi, sasa hivi taifa hilo limo kwenye mazingira yenye matumaini ya kufufua, kwa mafanikio, huduma za kiuchumi na kijamii nchini.