Ripoti mpya iliyotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF imesema kati ya mwaka 2005 na 2020 visa zaidi ya 266,000 vya ukiukwaji mbaya zaidi wa haki za watoto vimethibitishwa kutekelezwa na pande zote zinazohusika katika mizozo kwenye nchi zaidi ya 30, barani Afrika, Asia, Mashariki ya Kati na Amerika ya Kusini.