Balozi Johan C. Verbeke wa Ubelgiji, ambaye taifa lake limeshika madaraka ya uraisi wa Baraza la Usalama kwa mwezi Juni, aliwaambia waandishi habari wa kimataifa katika Makao Makuu kuwa kwamba anaashiria kuwepo “ajenda nzito” katika mijadala ya mwezi huu ya Baraza, na wingi wa mada zitakazozingatiwa kwenye Baraza, alisisitiza, zitahusu masuala ya Afrika.