Baada ya kufanyika mashauriano ya kiufundi, ya siku mbili, kwenye mji wa Addis Ababa, Ethiopia katika wiki hii, kati ya wawakilishi wa UM na wale wa kutoka AU, pamoja na wajumbe wa Serekali ya Sudan, kulidhihirika fafanuzi za kuridhisha juu ya yale masuala yaliokuwa yakikwamisha utekelezaji wa mpango wa kupeleka vikosi vya mseto kulinda amani katika jimbo la magharibi la Darfur. Baada ya kikao cha Addis Ababa kulitolewa taarifa ya pamoja kati ya Serekali ya Sudan na AU iliosema ya kuwa Sudan imeridhia na kuidhinisha ule mpango wa kupeleka vikosi vya mseto vya UM na AU kwenye jimbo la Darfur.