Mjadala wa ngazi za juu wa baolojia-anuai umeanza leo mjini Nagoya Japan. Mjadala huo unahudhuriwa na mawaziri wa mazingira kutoka takriban nchi 100, mashirika ya Umoja wa Mataifa kama lile la mazingira UNEP na Bank ya dunia.
UNCTAD inasema matumizi ya huduma na bidhaa zinazozalishwa nchini kunasaidia kutoa fursa za kazi zinazolipa vizuri na kuboresha kiwango cha maisha ya watu.
Wanawake wanaendelea kuwa na jukumu muhimu katika juhudi za kuleta amani amesema Bi Michelle Bachelete mkuu wa kitengo kipya cha Umoja wa Mataifa cha wanawake UN-Women.
Jopo la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa wanaoshughulika na upatikanaji elimu kwa wote. wametaja vipambele ambavyo vinaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa kupunguza pengo la kukosekana kwa usawa kwenye utoaji elimu.
Mtaalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa nchi kuwapa umuhimu wanawake kulingana na mipango ya kijamii hususan kwenye masuala ya kijamii.
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo amelaani vikali vitendo vya uvamizi vilivyofanywa dhidi ya askari wa amani wa Umoja wa Mataifa walioko katika eneo tete la mashariki mwa nchi hiyo.
Baraza kuu la usalama la Umoja wa Mataifa limeteua nchi 18 kuwa wanachama wa baraza la Umoja wa Mataifa lililo na jukumu kushughulikia masuala ya kimataifa ya kiuchumi na kijamii ECOSOC.
Athari za uharibifu uliosababishwa na kimbuga Megi baada yam vu za typhoon nchini Ufilipino zinaendelea kujitokeza na shirikisho la la kimataifa la chama cha msalaba mwekundu na mwezi mwekundu IFRC limetoa ombi la kimataifa la msaada wa dola milioni 4.3.